Jeshi
la Polisi Kitengo cha Kuzuia Dawa za Kulevya linamshikilia mkazi wa
Tabata Segerea Chama jijini Dar es Salaam Joseph Jaumbe( 52) kwa tuhuma
za kukutwa na dawa za binadamu kinyume na sheria huku zingine zikiwa
zimepita muda wake wa matumizi.
Akizungumza
leo jijini Dar es Salaam, Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi (ACP),
Alhaj Kabaleke Hassan amesema kupatikana kwa mtuhumiwa huyo kumetokana
na taarifa kutoka kwa wananchi kuwa anahifadhi dawa za kulevya ndipo
wakafanya uchunguzi na nyumbani kwake hakuwa na dawa za kulevya kama
walivyopata taarifa.
Amesema
baada ya uchunguzi ndipo wakakuta ana dawa za binadamu zikiwa katika
mifuko mbambali huku zingine zikiwa katika mfuko wa sandarusi.
Kamanda
Hassan amesema kuwa baada ya kuwasiliana na Mamlaka Chakula na Dawa
(TFDA) walipata dawa makopo 12 yenye vidonge 1000 ambazo hazijasajiliwa
na mamlaka hiyo, dawa za Serikali makopo mawili ya vidonge 1000 , dawa
zilizoisha matumizi yake uzito wa kilo 25, dawa bandia zilizoisha muda
wake makopo saba yenye vidoge 1000 , dawa za mashirika ya msaada makopo
12 yenye dawa 1000 kila kopo pamoja na vingashio za dawa mbalimbali.
Meneja
wa Kanda ya Mashariki ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Emmanuel
Alphonce amesema Jeshi la Polisi liendelee kufanya uchunguzi kwa mtu
huyo kujua dawa anakozipata ili kubaini mtandao huo.
Alphonce
amesema dawa hizo zingeingia mtaani zingeleta madhara kwa binadamu huku
akishangaa kwa dawa hizo kufungwa mfuko wa kiroba pamoja na mifuko ya
rambo.
Amesema
kuwa TFDA itaendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kuweza
kulinda watanzania katika matumizi ya dawa , vifaa tiba na vitendanishi.
Post A Comment: