Mkuu wa mkoa mstaafu Mzee Abbas Kandoro amefariki dunia usiku wa kuamkia leo  katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Jijini Dar alikolazwa kwa matibabu.

Kabla ya kifo chake aliwahi kuwa Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Arusha, Singida na Mbeya na mikoa mingine.

Siku mbili zilizopita Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alimtembelea na kumpa pole Mkuu huyo wa Mkoa Mstaafu, Abbas Kandoro ambapo awali alikuwa amelazwa katika hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma kabla ya kuhamishiwa Muhimbili Dar  ambapo umauti ndipo ulipomkuta.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: