Kikosi cha Simba kinaanza maandalizi yake rasmi leo kwa ajili ya mchezo dhidi ya watani wake wa jadi, Yanga, utakaopigwa Aprili 29 2018.

Simba ilirejea jana mjini Morogro kuweka kambi maalum kujiandaa na mechi hiyo ambayo huteka hisia za wapenzi na mshabiki wa soka nchini.

Kikosi hicho kilitua Morogoro jana baada ya kuvuna alama moja mjini Iringa dhidi ya Njombe kwenye mchezo wa ligi kuu baada ya matokeo ya sare ya 1-1.

Mpaka sasa Simba wapo kileleni mwa msimamo wa ligi wakiwa na alama 59 wakati watani zao wa jadi Yanga wana 48.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: