Mwanamuiki wa kike ambae pia ni mjasiriamali, Shiloleh ameonyesha tatoo aliyochora kwenye mwili wake yenye jina la mume wake mpendwa uchebe yenye jina ‘ASHRAF‘  na kusema kuwa hiyo ndio tatoo yake ya mwisho kuichora katika mwili wake.

Katika ukurasa wake wa instagram , Shilole aliandika;“Kwa mara ya kwanza na ya mwisho nimechora tatooooo ya jina la mume wangu Nampendaa sana”

Shilole aliwahi pia kuchora tattoo ya aliyekuwa mpenzi wake wa zamani Nuh Mziwanda na baadae kuifuta na hii itakuwa tattoo yake ya pili kuichora yenye jina la mwanaume ambae ni mpenzi wake na kuionyesha hadharani..
Share To:

msumbanews

Post A Comment: