Rais John Magufuli leo mchana Aprili 2,2018 anaweka jiwe la msingi la ujenzi wa mfumo wa rada za kuongoza ndege.
Mfumo
huo wa rada za kuongozea ndege unajengwa katika vituo vinne vya Uwanja
wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA); Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA); Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwanza
na Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Songwe.
Ujenzi
unafanywa na Kampuni ya M/S Thales Las France SAS ya nchini Ufaransa
ukigharimu Sh67.3 bilioni fedha zinazotolewa na Serikali ya Tanzania kwa
asilimia 100.
Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari
amesema leo Jumatatu Aprili 2,2018 kuwa ujenzi utakamilika ndani ya
miezi 18.
Amesema mradi huo utasaidia kurahisisha huduma za utafutaji na uokoaji kunapotokea ajali za ndege.
Johari
amesema pia utaiwezesha nchi kukidhi viwango na miongozo ya Shirika la
Kimataifa la Usafiri wa Anga (ICAO) na kujenga imani ya watumiaji wa
anga ya Tanzania.
Tayari wageni wamewasili eneo la uzinduzi wakiwamo mawaziri, wabunge, mabalozi na wananchi.
Mkuu
wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewasili akiongozana na msanii
wa muziki wa kizazi kipya Naseeb Abdul maarufu Diamond.
Post A Comment: