Mwili wa mama mzazi wa RC wa Arusha, Mrisho Gambo, Rehema Paulo Momburi aliyefariki, April 13, nchini India utawasili leo April 17, 2018 , Jumanne.

Mara baada ya kupokelewa katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JNIA Dar es Salaam, mwili utapelekwa hospitalini kwa ajili ya kuhifadhiwa hadi kesho, Jumatano ambapo utaagwa nyumbani kwake Kariakoo, karibu na Shule ya Sekondari ya Benjamin Mkapa kuanzia saa 3 asubuhi.

Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu, Mkuu wa mkoa wa Arusha, amesema mwili wa mama yake utasafirishwa kesho jioni kwenda Arusha kwa ajili ya Duwa siku ya Alhamisi na kisha atazikwa katika makaburi ya Moshi URU
Share To:

msumbanews

Post A Comment: