Msanii wa Muziki Bongo, Amber Lulu amefunguka kuhusu mipango yake ya kuolewa.

Muimbaji huyo ambaye yupo katika mahusiano na rapper Prezzo kutoka nchini Kenya, amesema ndoa ni majaliwa ya Mwenyenzi Mungu ila anaamini muda wowote ataolewa.
“Ndoa ni majaliwa kwa hiyo any time, Mungu akitujalia mtaona nitavaa sana shela,” amesema Amber Lulu.
Hata hivyo amekiri kuwa hajawahi kutambulishwa au kufika nyumbani kwa Prezzo kwani msanii huyo mara nyingi ndiye amekuwa akija hapa nchini.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: