Bado ni drama tele kati ya Nandy na Bill Nass, safari hii mpenzi wa Bill Nass amemshukia vikali Nandy kwa kile kilichotokea.

Alice ambaye ndiye anadaiwa kuwa katika mahusiano na Bill Nass kwa sasa ameonyesha kutopendezwa kabisa na kile kilichotokea kwa mpenzi wake pamoja na Nandy. Kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika;

Ujue wakati mwingine jitahidi kujiheshimu Nandy, Ulimpigia William simu ukimuomba akutumia picha zenu za wakati mnadating…. bila hiyana mume wangu alikutumia, lakini wewe uliposti zile picha hukuridhika ukaamua uachie video chafu kama ile halafu hapo hapo unakataa na kumlaumu mume wangu wakati iliyotumika ni simu yako.

Upande wako kama unaona umewin basi jua umetuharibia mimi na mume wangu sana na hata kwa watoto wetu huko mbeleni sijui watamjengea picha gani baba yao.

Cant you doing your fu*** music bila kiki?, au uliona mume wangu William ndo wa kutafutia kiki, naomba ukome tena haswa, kama ulikuwa naye ndio ishapita hivyo tuache na mahusiano yetu, sijui ni mwanamke wa dizaini gani wewe usiyekuwa na haya, unayejua kuvaa nje, ndani hujui, ile chu** ni ya kuvaa msichana kama wewe.

Hapo juzi, April 12, 2018 ilivuja video mtandaoni ya utupu ambayo iliwaonyesha Bill Nass na Nandy wakiwa faragha. Nandy ameshaomba radhi kwa mashabiki wake kutokana na tukio hilo na kueleza hajui nani hasa amevujisha video hiyo ila amekiri kuwa yeye ndiye aliirekodi
Share To:

msumbanews

Post A Comment: