Wakati Wabunge walikuwa wakichangia mapendekezo yao katika  bajeti ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2018/19   Mbunge wa viti maalum CCM Hawa Mchafu Chakoma  ameishauri serikali kuanzisha namna bora ya  mpango wa pensheni kwa wazee waliolitumikia taifa.

Hawa Mchafu alisema ;"Nashindwa kufahamu mfuko wa moja kwa moja ambao upo kwa ajili ya wazee, muda umefika sasa ule mchakato wa pensheni kwa wazee uje sasa ili kuweza kuwasaidia wazee wa taifa letu ambao kwa nafasi zao walisaidia sana nchi yetu”

“Niipongeze Serikali pia kwa kuanzisha miradi mbalimbali mikubwa ikiwemo ujenzi wa bomba la mafuta, ujenzi wa viwanja vya ndege n.k  ....ni wazi itaambatana na upatikanaji wa ajira lakini niishauri Serikali ihakikishe inafuatilia mikataba ya kazi kwa watanzania inayofanyika katika miradi hiyo kwamaana kumekuwa na ukakasi mkubwa sana mikataba mingi inaukiukwaji wa kisheria” –Hawa Mchafu
Share To:

msumbanews

Post A Comment: