Mbunge wa Ulanga (CCM), Gudluck Mlinga ameomba mwongozo wa Spika bungeni akitaka kujua namna chombo hicho cha Dola kinavyoweza kuzuia wanawake waliofika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa madai ya kutelekezwa na watoto wao.

Mlinga ameomba mwongozo huo leo Jumatano Aprili 11, 2018 akisema kitendo hicho kinawadhalilisha watoto ambao hufika katika eneo hilo wakiwa na mama zao, akidai kuwa kinavunja Katiba ya nchi.

Mwongozo huo uliibua kelele bungeni baada ya mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga kutoa majibu kwamba suala hilo ni la kisheria, kupingwa na wabunge waliohoji sheria ipi.

Mlinga alitaka kujua namna ambavyo Makonda anavyovunja Katiba kwa kuanika mambo ya siri hadharani jambo ambalo linakwenda kinyume na Katiba, akitaka Bunge liingilie kati na kukemea kitendo hicho.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: