Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana amkutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa nchini Uingereza  Mhe. Penny Mordaunt .

Makamu wa Rais yupo  nchini Uingereza   kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa Serikali wa Jumuiya ya Madola (CHOGM) akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli.

Katika mkutano wake na Waziri huyo wa Uingereza Makamu wa Rais alielezea hatua kubwa iliyofikiwa na Serikali ya Awamu ya Tano katika Elimu mara baada ya kuamua Elimu iwe bure kuanzia darasa la kwanza mpaka kidato cha nne.

Pia Makamu wa Rais alishukuru mradi wa DFID unatekelezwa mkani Simiyu na kuomba mradi huo uongezewe maeneo ili uweze kuwanufanisha watoto wengi wa kike.

Makamu wa Rais pia alizungumzia namna Majukwaa ya Kuwawezesha wanawake kiuchumi yanavyofanya kazi huku taratibu mbali mbali zinafanyika ili mabenki yaweze toa mikopo kwa riba nafuu.

Mwisho Makamu wa Rais alizungumzia jitihada mbali mbali zinazofanywa na Serikali katika kuboresha Mazingira ya kufanya Biashara nchini.

Naye Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa nchini Uingereza Mhe. Penny Mordaunt ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa jitihada wanazofanya katika kuboresha huduma za kijamii, alisema nchi yake ipo tayari kusaidia katika masuala ya makusanyo ya kodi, kuboresha uwezo wa walimu kwa kuwapatia mafunzo mbali mbali.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: