Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Kheri James amefunguka hatima ya Wema Sepetu na Jokate Mwegelo ndani ya umoja huo.
Akizungumza leo Kikaangoni, EATV amesema hawezi kujibu kuhusu Jokate kuondolewa UVCCM kwa sasa.
“Kama ambavyo hatukuwaeleza sababu za kuteuliwa kwake Jokate ndivyo ambavyo hatutawaambia sababu za kutolewa kwake” amesema.
“Wema mimi simjui namsoma tu kwenye magazeti, amerudi CCM lakini si UVCCM,” amesisitiza.
March 25 mwaka huu Kamati ya Utekelezaji ya UVCCM ilitengua uteuzi wa aliyekuwa Kaimu Katibu wa Hamasa na Chipukizi wa umoja huo, Jokate Mwegelo.
Pia utakumbuka February 24, 2017  Wema alijiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) akitokea Chama cha Mapinduzi (CCM) December 01, 2017 alitangaza kurejea CCM.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: