Naibu Katibu Mkuu Dk. Ave maria Semakafu akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wadau kuhusu haki za mtoto, mkutano ambao umefanyika jijini Dar es salaam.
Wageni waalikwa katika meza kuu wakifuatilia majadiliano kupitia jukwaa la kutetea haki za mtoto.

Baadhi ya wajumbe wa mkutano unaojadili haki za mtoto wakisikiliza kwa makani hotuba ya Naibu katibu Mkuu Dk. Semakafu (hayupo pichani) wakati akifungua mkutano huo jijini Dar es Salaam.


Serikali ya awamu ya Tano  imesema katika kulinda haki za mtoto imedhamiria kujenga shule za Elimu Jumuishi na zile za  wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika kila mkoa.

Kauli hiyo imetolewa na  Naibu Katibu Mkuu wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk. Ave maria Semakafu jijini Dar es Salaam wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa wadau unaojadili haki za mtoto.

Dk. Semakafu amesema lengo la ujenzi wa shule hizo ni kuhakikisha watoto wote wa kitanzania wapata Elimu bila vikwazo vya aina yoyote kwani Elimu ni msingi wa Maenedeleo.

Amesema katika kutekeleza hilo tayari Wizara hiyo inajenga shule ya mfano kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu katika chuo cha Ualimu Patandi kilichopo mkoani Arusha, ambapo shule hiyo itakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi wa shule ya msingi mpaka Sekondari.

Naibu Katibu Mkuu huyo amewataka wazazi kuhakikisha wanawapeleka watoto wote wenye umri wa kwenda shule bila kuangalia changamoto za kimaumbele walizonazo watoto wao kwa kuwa tayari Serikali imewekeza katika eneo hilo.

Mwakilishi wa UNICEF katika masuala ya Elimu nchini Tanzania Cecilia Baldeh amesema tayari Tanzania imekwisha piga hatua katika kulinda na kutetea haki za mtoto ikiwa ni pamoja na Serikali kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanakwenda kwa kuwa Elimu msingi hivi sasa inatolewa bure.

Imetolewa na;
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
6/04/2018




Share To:

msumbanews

Post A Comment: