Abednego Damian ‘Belle 9′
MKALI wa Bongo Fleva, Abednego Damian ‘Belle 9′ ndiye ‘aliyembatiza’ jina la Masogange mrembo maarufu wa kuuza sura kwenye video za wasanii, marehemu Agness Gerald.
Kabla hawajakutana na kumuuzisha sura kwa mara ya kwanza katika wimbo wake wa Masogange, wengi walikuwa hawamfahamu Masogange, lakini baada ya wimbo huo, kila mmoja aliweza kumjua kutokana na kuutendea haki wimbo huo.

Mbali na kuuza sura, Masogange alikuwa na sifa ya ziada iliyowafanya wasanii wengi wavutiwe kufanya naye kazi. Muonekano wake ulikuwa kivutio kikubwa na hapo ndipo umaarufu wake ulipozidi kushika kasi kama moto wa kifuu.
Katika makala haya, tumezungumza na Belle 9 ambaye amefunguka mambo mengi kuanzia walipokutana, hadi kufanya video yake ya Masogange na jinsi alivyoguswa na kifo chake kilichotokea Aprili 20, mwaka huu katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge jijini Dar:
Share To:

msumbanews

Post A Comment: