Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda amepiga marufuku baadhi ya watendaji wanaozuia Wasanii kurekodi Video za Nyimbo au Movie kwenye mandhari (location) mbalimbali za jiji hilo kwakuwa   linalorudisha nyuma Utalii.

Haiwezekani msanii akitaka kurekodi Video au Movie kwenye mitaro ya maji machafu ambayo inatoa taswira mbaya kwa jiji letu hasumbuliwi vibali lakini akirekodi kwenye Hotel, Majengo Marefu, fukwe au kwenye mazingira mazuri anasumbuliwa kibali,  hili haliwezekani, kuanzia sasa wasanii mtarekodi Video Location yoyote mnayotaka isipokuwa Ikulu, Mahakama, Maeneo ya jeshi na vituo vya polisi ambapo panahitaji vibali maalumu* Alisema RC Makonda.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: