Baadhi ya wananchi wa Mtaa wa Nyakabale wilayani Geita wametelekeza mwili wa marehemu nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa huu, Elias Ndarawa.
Ndarawa anatuhumiwa kutoshughulikia tukio la Zacharia Shaban kupigwa na polisi jamii hadi kufa.

Wananchi hao waliubeba mwili wa Zacharia na kuulaza kwenye kitanda cha mwenyekiti huyo.

Majaliwa Shaban ambaye ni ndugu wa marehemu Zacharia amesema leo Machi 12,2018 kwamba nduguye alipigwa Machi 5,2018 akiwa eneo la Mgodi wa Dhahabu Geita (GGM) akiokota mabaki ya mawe ya dhahabu maarufu magwangala.

Amesema Zacharia alipelekwa polisi alikokaa kwa siku sita na aliporudi uraiani hali yake ilikuwa mbaya.
Majaliwa amesema nduguye alipelekwa hospitali alikofariki dunia Jumamosi Machi 10,2018 na hadi sasa hakuna kiongozi aliyefika kwenye msiba huo wala kutoa kauli yoyote.

Mkazi wa mtaa huo, Johnson John amesema hawapo tayari kuzika hadi Serikali itakapotoa kauli kuhusu hatima ya maisha yao kwa kuwa polisi jamii wamekuwa wakiwapiga na kuwajeruhi.

Jana, Machi 11,2018 wananchi walivamia eneo la kituo cha polisi jamii kilichopo mtaa wa Manga na kukichoma moto kwa madai kwamba wamempiga na kumuua Zacharia

Share To:

msumbanews

Post A Comment: