MAMA mwenye mtoto mwenye nguvu za ajabu anayeishi Mtaa wa Kwa Mbela uliopo Mburahati Mianzini Salama Omar amemuomba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda kumsaidia katika matibabu ya mwanaye.

Mbali ya kumuomba Makonda kumsaidia matiabu ya mtoto wake Mzamiry Said(7), pia ametumia nafasi hiyo kuelezea namna ambavyo mumewe aliyefunga naye ndoa mwaka 2009 alivyomtekeleza yeye na mtoto.

Akizungumza na Michuzi blog leo jijini Dar es Salaam Salama amesema anaishi maisha yenye changamoto nyingi anakabiliana nazo katika malezi ya mtoto wake ambaye ameeleza amekwenda kwenye hospitali mbalimbali ikiwemo Hospitali ya Taifa  Muhimbili na CCBRT.

Amefafanua na kote huko alikokwenda madaktari wamechukua vipimo vyote vikiwemo vya kuangalia iwapo ana tatizo la akili au ulemavu lakini wamemthibitisha matatizo hayo ila anakumbuka mmoja wa madaktari wa Muhimbili anayeshughulikia watu wenye magonjwa ya akili anakumbuka alimwambia mwanaye hata pona , hivyo ataendelea kuwa hivyo katika maisha yake yote.

"Ni kweli mwanagu sasa ana maiaka saba na tatizo bado lipo.Ana nguvu nyingi na anapocheza na wenzake unakuwa makini kufuatilia maana anaweza kufanya chochote ambacho si kizuri. Napata shida kwenye malezi ya mwanangu tangu alipozalizwa.

Nimejitahidi katika matibabu lakini hali iko vile vile.Muda wote inabidi niwe namchunga asiende mbali kwani unaweza kumuacha akaenda kucheza na watoto wengine mtaani lakini kutokana na nguvu alizonazo anaweza hata kujeruhi.

"Kuna wakati anaweza kukaa lakini ghafla ukamuona anaanza kukimbia ,hivyo ili nimshike natumia nguvu nyingi sana maana anaweza kunishika mkono na nikashindwa kuutoa.Kote mtaani hadi Serikali za mitaa wanamjua na matatizo yanayomkabili.Kwa kweli nahangaika sana na malezi ya mtoto, sina wa kunisaidia na kwa kuwa muda wote nipo nakosa hata nafasi ya kwenda kutafuta fedha kwa ajili ya 
kula.

"Moyo wangu unanisukuma na kuamini Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam atanisaidia na nipo tayari kupokea msaada wa aina yoyote atakaoamua kunisaidia iwe matibabu au chakula .Makonda ni kiongozi anayeguswa na shida za watu na naamini hata mimi akisikia kama taarifa hizi ataziona naomba anisaidie na Mungu atamlipa kwa kile ambacho atakifanya kwa ajili ya wanangu,"amesema Salama.

 "Kuhusu hili la mume wangu kunitelekeza na mtoto, natamani kwenda kwa Makonda pia kwa ajili ya kupata maada wa kisheria kwani tangazo lake la kuagiza wanawake waliotelekezwa na waume zao waende kwake nimelisikia lakini sasa sina mtu wa kumuachia mtoto.

"Mkuu wangu wa mkoa naomba nisaidie ili itoke kwenye changamoto za kimaisha.Mtoto aahitaji eneo lenye utulivu kwani akiona watu ndio kama vile anachanganyikiwa na nguvu za ajabu zinamjia,"amesema.

 Kuhusu aina ya maisha ambayo anaishi kwa sasa anasema bado anaendelea kutafuta matibabu kwa ajili ya mwanaye kwani hajakata tamaa na anaamini ipo siku Mungu atamuondolea maradhi na kusisitiza anaamini msaada wa Makonda iwapo atamsikia anaweza kumsaidia.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: