Kamati ya maadili ya TFF, imemfungia kifungo cha maisha kutojihusisha na shughuli za soka Makamu Mwenyekiti wa shirikisho hilo, Michael Wambura.
Wambura amekutana na adhabu hiyo nzito kutokana na kupokea fedha zisizo halali kiasi cha shilingi milioni 84 na makosa mengine matatu.
Makaosa hayo mengine matatu aliyokutwa nayo Wambura, ni kugushi nyaraka za malipo ya fedha, na kula njama kulipwa fedha na waliokua viongozi wa TFF Malinzi na Mwesigwa.
Kamati hiyo ya maadili imefikia maamuzi hayo kwenye kikao chao walichokutana jana (Jumatano).
Share To:

msumbanews

Post A Comment: