Madiwani wa Chadema mkoani Arusha waliojiuzulu na kujiunga na CCM wamefikia 21 baada ya Jana Machi 11,2018 Elirehema Nnko wa Kata ya Osunyai kujiuzulu akiunga mkono jitihada za Rais John Magufuli.

Nnko ambaye ni wa tano kujiuzuru katika Halmashauri ya Jiji la Arusha amesema amefikia uamuzi huo katika kumuunga mkono Rais kwa kuwa hakuna kazi anayofanya sasa katika kambi ya upinzani.
Amesema alipokuwa Chadema alikosa ushirikiano katika kutimiza majukumu yake kutoka kwa viongozi wa chama hicho.

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Athuman Kihamia amekiri kupokea barua ya kujiuzulu Nnko na kwamba utaratibu wa kupeleka taarifa Tamisemi umeanza.
Amesema Nnko katika barua hiyo ameeleza hajashawishiwa kujiuzulu bali anaunga mkono utendaji kazi mzuri wa Rais Magufuli.

Katika Halmashauri ya Jiji la Arusha madiwani waliojizulu ni watano; Monduli (mmoja); Longido (watatu); Meru (sita); na Ngorongoro (sita).

Akizungumzia kujiuzulu kwa madiwani, Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema hakutakiua chama hicho.

Meya wa Jiji la Arusha, Kalist Lazaro amesema madiwani waliojiuzuru walitokana na mafuriko ya mwaka 2015 na walikuwa hawajui joto la kuwa kiongozi wa upinzani.

"Waache waondoke jiji tulikuwa madiwani 33 wa Chadema sasa wameondoka watano haitupi shida," amesema Lazaro.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: