Picha inayohusiana
Roma Mkatoliki na Mkewe

Kila mdau wa muziki nchini Tanzania kwa sasa anahamu ya kusubiri wimbo mpya wa rapa Roma Mkatoliki hii baada ya mkali huyo wa Hip Hop kupitia katika kipindi kigumu cha kufungiwa wimbo wake na yeye mwenyewe kupigwa marufuku ya kutojihusisha na muziki.
 
Sasa habari nzuri ni kwamba jina la wimbo wake mpya ambao unatarajiwa kuachiwa limeshavuja na sio lingine ni  “NIKIFA CHIMBENI MAKABURI MATATU” jina ambalo limevujishwa na mkewe.
Mkewe na Roma Mkatoliki, Nancy amesema anajua magumu anayopitia mumewe na anawaza endapo ataachia wimbo huo wa “NIKIFA CHIMBENI MAKABURI MATATU” maisha yake yatakuwaje? kwani ugumu wa mashairi yaliyomo kwenye wimbo huo yanamtia hofu.
Dah Nawazaa Sijui Baba Ataimba Nini Sasa Round hii! Kila Angle Wanakukazia!! Nawaza Ukiachia Ile “NIKIFA CHIMBENI MAKABURI MATATU.“ameandika Mke wa Roma kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Hata hivyo, Nancy amemshauri Roma asiuachie wimbo huo kwani bado anampenda na anahofia kumpoteza.
Lakini Daaah Bora Ukae Kimya Tu!! Bado Nakuhitaji Mume Wangu!! Nways Tutege Sikio Tu!!“ameandika Nancy.
Kwa upande mwingine, Mashabiki na wadau wa muziki wametoa maoni yao ambapo kila mmoja ameonekana kumsapoti mkewe na Roma wengine wanataka wimbo huo utoke.
  • saidipeter24 Bora akae kimnya coz hali si shwari
  • 16_geniuz_paranawe ROMA ni kichwa. Ana vingi vya kuimba. Na kimsingi hakuna sababu y kumuwazia kwan ataimba1nin.Jamaa ana akili nyingi sna.
  • __ambrseBora Kwa kipind hiki aache tu maana wote bado tunamhitajilabda aimbe kwaya tu kama anaweza
  • tmpya Mwmabie asiwe muoga,Kina mandela,nyerere Nk wangekua waoga leo tusngekua hapa.
  • apologizekii Natamani Nikuunge mkono ila pia na tamani kusikia ladha ya baba
  • financial9870 Mbona zamani alikua anaimba vzr tu sa hyo kibamia ikipigwa kwenye daladala tunaoneana aibu ikipigwa tupo na famil tunabadili stesheni ikipigwa niko na baby kibamia anahisi namdedicat raha iko wapi?
Alhamisi ya  Machi 29, 2018 Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Harrison Mwakyembe alitangaza kumfutia adhabu ya kifungo cha miezi sita rapa Roma Mkatoliki alichopewa na Naibu Waziri wa wizara hiyo Juliana Shonza.
Hakuna asiyefahamu makali ya ngoma za Roma Mkatoliki na wewe mdau wa muziki una lipi la kumshauri Roma Mkatoliki kwa jinsi unavyoona jina la wimbo huo?
Share To:

msumbanews

Post A Comment: