Mkuu wa wilaya ya Muleba Mhandisi Richard Ruyango ameliagiza jeshi la polisi katika wilaya hiyo kumkamata na kumfikisha mahakamani Mganga wa zahanati ya Kibanga wilayani humo Ruiz Polepole.

Mkuu wa Wilaya huyo ametoa agizo hilo kufuatia wananchi wa kijiji cha Kibangu kutega mtego ambao ulimnasa Mganga huyo wa zahanati ya Kibanga akiuza dawa zinazotolewa na Serikali ambazo zinapaswa kutolewa bure.

Aidha upelelezi ukikamilika mganga huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo za kuuza dawa za serikali kinyume na utaratibu wa serikali.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: