Baada ya siku ya uvumi wa siku nyingi, imethibitishwa kwamba kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amezuru China.

Ziara hiyo, ambayo ilithibitishwa na China na Korea Kaskazini, ndiyo ya kwanza inayofahamika ya Bw Kim nje ya taifa lake tangu alipochukua mamlaka mwaka 2011.

Bw Kim alifanya "mazungumzo ya kufana" na kiongozi wa China Xi Jinping mjini Beijing, shirika la habari la China, Xinhua liliripoti.

China ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini kiuchumi na baadhi ya wachambuzi wanasema uwezekano wa wawili hao kabla ya mkutano mkuu wa Bw Kim na viongozi wa Korea Kusini na Marekani ulitarajiwa.

Bw Kim amepangiwa kukutana na Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in mwezi Aprili na Rais wa Marekani Donald Trump mwezi Mei.

Ziara hiyo ya Beijing inatazamwa na wengi kama hatua muhimu katika maandalizi ya Korea Kaskazini kuhusu mazungumzo hayo.

Wakati wa ziara hiyo, Bw Kim alimhakikishia mwenzake wa China kwamba amejitolea kuacha kustawisha silaha za nyuklia, kwa mujibu wa shirika la habari la Xinhua.

Hata hivyo, alisema atafanya hivyo bila masharti.
"Suala la kumalizwa kwa silaha za nyuklia katika Rais ya Korea linaweza kutatuliwa, lakini iwapo tu Korea Kusini na Marekani watajibu juhudi zetu kwa nia njema, kuunda mazingira ya amani na uthabiti na pia kwa kuchukua hatua za kusonga mbele kwa pamoja kutoka kwa wadau wote kuhakikisha amani inapatikana," Bw Kim alinukuliwa akisema.

Uhusiano na Beijing
Shirika la habari la Korea Kaskazini, KCNA, lilieleza ziara hiyo kama yenye umuhimu mkubwa katika kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na China.

"Ina maana kwa Korea Kaskazini kufafanua msimamo wake na kushirikiana na China, mshirika wake muhimu zaidi," msomu katika Pacific Forum CSIS Andray Abrahamian ameambia BBC.

"Uhusiano huo umekuwa ukidhoofika katika miaka mitano iliyopita na China imekuwa imetengwa kidiplomasia katika miezi kadha iliyopita," amesema.

"Kutoka kwa mtazamo wa Beijing, hii ni ziara ambayo ilifaa kufanyika kitambo sana."

Kwa sehemu kubwa, hii ni ziara yenye maana kubwa kwa urafiki wa Korea Kaskazini na China, na ni ishara ya heshima pia, Fyodor Tertitskiy wa shirika la habari la NK News linaloangazia sana taarifa kuhusu Korea Kaskazini alisema.

"Wana mikutano miwili mikubwa kati ya kiongozi wao na mataifa mengine - mmoja na Seoul na mwingine na Washington - na pengine wanataka kuusikia msimamo wa China pia.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: