Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr,John Pombe Magufuli amemuagiza Waziri wa TAMISEMI Seleman Jafo kuwasimamisha kazi Wakurugenzi wawili wa Kigoma Ujiji na Pangani kwa sababu ya kupata hati chafu katika ripoti ya CAG iliyowasilishwa leo.

“Kuna Wilaya mbili, Halmashauri Mbili zina hati chafu, Mimi nafikiri Kigoma Ujiji na Pangani, Mimi nafikiri saa nyingine tuchukue hatua kwa vile Waziri wa TAMISEMI upo hapa WAKURUGENZI wa Wilaya hizo WASIMAMISHWE kazi leo” -Rais Magufuli
Share To:

msumbanews

Post A Comment: