BARAZA la Sanaa Tanzania (BASATA) limemfungia Rapa Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’ kwa muda wa miezi sita kutojihusisha na sanaa ya muziki kutokana na kutotii agizo la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo lililomtaka kubadilisha maudhui ya wimbo wake wa KIBAMIA.

Kutokana na wimbo huo ambao Roma amewashirikisha wasanii wenzake, Stamina na Maua Sama, Basata walimuita na kumweleza arekebishe maudhui ya wimbo lakini inasemekana hakutekeleza agizo hilo hivyo BASATA wameamua kumfungia.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: