Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo, ambaye pia ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aliyekuwa hajulikani alipo tangu usiku wa kuamkia jana, amepatikana Mafinga mkoani Iringa.

Jeshi la Polisi mkoani humo kupitia kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Juma Bwire amethibitisha kupatikana kwa mwanafunzi wa UDSM, Abdul Nondo wilayani Mufindi na sasa yupo katika Kituo cha Polisi Mafinga akitoa maelezo.
Inasemekana Abdul Nondo amejikuta ametupwa pembezoni mwa barabara
Share To:

msumbanews

Post A Comment: