Msanii wa muziki Bongo, Chege amengufuka kuhusu mipango yake ya kuoa.

Chege ambaye leo ameachia ngoma mpya ‘Kaitaba’ aliyomshirikisha Saida Karoli ameiambia Clouds Fm kuwa atakuwa wa mwisho kuoa kwani hapendi kushauriwa kitu baada ya watu wengine kufanya kitu kama hicho.
“Huwa sipendi kuambiwa nifanye kitu ambacho mwingine amekifanya, nina mpenzi ninayempenda kabisa na tunaishi pamoja, muda ukifika nitaoa, nilichogundua nitakuwa wa mwisho kuoa” amesema Chege.
September mwaka jana Chege aliiambia Bongo5 kuwa kitendo cha kuoa ni kujifunga milele, hivyo mtu anatakiwa achague mwenza sahihi ambaye anaweza kuishi naye kwa muda wote huo na isiwe kuoa kwa sababu ya trending za watu kitu ambacho hawezi kukipa nafasi katika maisha yake.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: