Klabu ya Manchester United imefanikiwa kurudi nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi Kuu England (EPL) kwa kuitafuna klabu ya Chelsea goli 2-1.
Lukaku na Jesse Lingard
Chelsea walikuwa ndio wa kwanza kuliona langu la United kupitia kwa Wilian kunako dakika 32 kabla ya Romelu Lukaku kusawazisha kunako dakika ya 39 na hadi mapumziko timu zote zilikuwa 1-1.
Goli la ushindi la United limefungwa na kinda, Jesse Lingard kunako dakika ya 75 hadi filimbi ya mwisho inalia, Man United 2 Chelsea 1.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: