Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akizungumza na wananchi wa Kahama mkoani Shinyanga mara alipowasili katika wilaya hiyo kwa ziara ya kikazi ya kuzungumza na maofisa na askari wa Jeshi hilo, IGP Sirro amewataka wananchi hao kuendelea kutoa ushirikiano kwa Jeshi hilo pamoja na kuwafichua wahalifu waliopo kwenye maeneo yao.
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia mkoa wa Shinyanga, wakiimarisha ulinzi wakati Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, aliposimamisha msafara wake ili kuzungumza na wananchi waliojitokeza barabarani katika mji wa Kahama mkoani Shinyanga leo.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga Simon Haule (aliyesimama) akitoa hotuba mbele ya Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, aliyewasili mkoani humo kwa ziara ya kikazi yenye lengo la kuzungumza na Maofisa na askari wa Jeshi hilo na kuwakumbusha kutimiza wajibu wao wa kutenda haki kwa wananchi wanaowahudumia.
Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro, akiwa katika picha ya pamoja na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia wa mkoa wa Shinyanga leo akiagananao mpakani mwa mkoa huo na wilayani Mbogwe, Geita, IGP Sirro yupo mkoni humo kwa ziara ya kikazi. Picha na Jeshi la Polisi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: