February 17 ni siku ambayo jimbo la Siha mkoani Kilimanjaro kulifanyika uchaguzi mdogo na mgombea Ubunge kupitia tiketi ya CCM Dr Godwin Mollel alifanikiwa kuibuka mshindi wa Ubunge kwa kupata jumla ya kura 25611.

Leo baada ya ushindi huo ameamua kupita kwenye kata nne kwa ajili ya kushukuru na kusema kuwa hatofanya sherehe kama wabunge wengine wanavyofanya baada ya kutangazwa washindi, bali atafanya shughuli za maendeleo kama sehemu ya sherehe yake.

Dr Mollel katika kata ya Nduimet ameahidi kutoa mabati 200 yatakayosaidia kukamilisha ujenzi wa darasa la shule ya Lemushu, akiwa anaendelea na zoezi hilo amepita pia kwa viongozi wa dini na kuahidi kushirikiana nao baada ya kutembelea kata za Nduimet, Engaranairobi, Sanya Juu na kata ya Lawate.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: