Basi la abiria (Daladala) linayofanya safari zake kati ya Mbezi na Makumbusho jijini Dar es Salaam limepinduka leo Jumatatu, Februari 26, 2018 asubuhi katika eneo la Kimara Korogwe.

Polisi wapo eneo la tukio kufanya jitihada za kuokoa watu waliokuwemo kwenye ajali hiyo ambapo basi limepinduka na kugeuka magurudumu yakawa juu.

Idadi ya majeruhi haijajulikana na iwapo kuna watu waliopoteza maisha kwenye ajali hiyo. Tutakupa taarifa zaidi baadaye.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: