Mwanafunzi wa chuo Kikuu cha Nairobi nchini Kenya amemfungulia mashtaka mfanyakazi wa Bunge la nchi hiyo, kwa kutaka kumlawiti
Mfanyakazi huyo ambaye jina lake limehifadhiwa kwa ajili ya usalama wake, ametajwa kutaka kumfanyia kitendo hiko kiovu mwanafunzi wa kiume, kwenye maeneo ya ofisi za bunge.
Kwenye maelezo yake mwanafunzi huyo amesema kwamba afisa huyo alimfuata na kumwambia yeye ni Afisa wa Polisi, na kumchukua mpaka ndani ya majengo ya bunge, na kuanza kumfanyia vitendo hivyo viovu.
“Aliniafuata na kunikamata akiniambia yeye ni polis, akanipeleka ndani ya jengo la bunge, na kuanza kugusa na kuniingiza uum* wake sehemu zangu za nyuma za siri..”, alikuwa akielezea mwanafunzi huyo ambaye jina lake limehifadhiwa pia.
Hata hivyo tetesi zinasemekana kuwa muhanga wa tukio hilo alikubali kufuta kesi mahakamani, baada ya kupewa rushwa ya shilingi elfu 5 ya Kenya, amabyo ni sawa na shilingi laki moja ya Tanzania. Source Citizen
Share To:

msumbanews

Post A Comment: